15 Juni 2015 - 21:10
Watunis wanane watekwa mjini Tripoli

Radio ya serikali ya Tunis imetangaza kutekwa wananchi wanane wa nchi hiyo siku ya Jumapili nchini Libya, wananchi ambao walikuwa kikazi nchini Libya na kutekwa katika mji mkuu wa nchi hiyo.

Shirika la habari AhlulBayt (a.s) ABNA: habari za kutwekwa kwa watu hao zimeenea katika hali ambayo watu wenye silaha wamewateka watu 10 siku ya Ijumaa ambao ni wafanyakazi wa ubalozi wa Tunis nchini Libya.
Taarifa zasema kuwa mpaka sasa hakuna kikundi chochote kilichodai kuhusika na tukio hilo.
Libya toka baada ya kuanguka utawala wa Gaddafi dikteta wa nchi hiyo mwaka 2011 mpaka sasa kuna hali mbaya ya kugombania madaraka na kushika nafasi ya Gaddafi.